Have any question?
+255 736 164 141
info@libertysparks.org
RegisterLogin
DONATE
  • About Us
    • Our Story
    • What we do
    • People
    • Jobs & Internships
    • Annual Reports & Financials
    • FAQs
    • Contact
  • Partners
  • Training
    • Overview
    • Certifications
    • Upcoming Courses
    • Think Tank Shark Tank
    • FAQs
  • Grants + Awards
Menu
  • About Us
    • Our Story
    • What we do
    • People
    • Jobs & Internships
    • Annual Reports & Financials
    • FAQs
    • Contact
  • Partners
  • Training
    • Overview
    • Certifications
    • Upcoming Courses
    • Think Tank Shark Tank
    • FAQs
  • Grants + Awards
  • News+Analysis
  • Media
    • Books
    • Videos
    • Champions of Change
  • Events
  • Support us
Menu
  • News+Analysis
  • Media
    • Books
    • Videos
    • Champions of Change
  • Events
  • Support us

Blog

Vodacom kutotoa gawio baada ya kupata hasara

  • Posted by Admin
  • Categories Blog, Business, News
  • Date July 20, 2021
  • Comments 0 comment

Dar es Salaam. Bodi ya Wakurugenzi ya kampuni ya simu ya Vodacom imesema hakutakuwa na gawio kwa wanahisa katika kipindi cha mwaka wa fedha ulioishia Machi, 2021.

Sababu za kutotolewa kwa gawio hilo ni hasara ya Sh30 bilioni iliyopatikana katika kipindi hicho na hii inakuwa mara ya kwanza kutotolewa kwa gawio tangu kampuni hiyo iorodheshwe katika soko la hisa la Dar es Salaam (DSE) Agosti 2017.

“Kutokana na hasara iliyopatikana baada ya kulipa kodi, bodi ya wakurugenzi imeamua kutopendekeza gawio katika kipindi hicho cha mwaka wa fedha ulioishia Machi 31, 2021,” ilieleza taarifa ya kampuni hiyo ya hesabu za awali.

Katika taarifa hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom, Hisham Hendi alisema hasara hiyo inatokana na namna kodi ilivyokokotolewa na kusababisha kutozwa kiwango kikubwa tofauti na mwaka uliopita.

Pia alibainishwa suala la kufungwa kwa laini milioni 2.9 za wateja wao ambao hawakukamilisha usajili liliathiri mapato na faida ya kampuni hiyo.

Katika kipindi cha mwaka wa fedha uliopita (ulioishia Machi, 2020) Vodacom ilipata faida halisi ya Sh45.76 bilioni ikipungua kutoka Sh90.76 bilioni iliyopatikana kwa mwaka ulioishia Machi, 2019.

Faida ya mwaka 2020 ilipungua kutokana na kuongezeka kwa gharama za kuhakikisha wateja wote wanasajiliwa kwa alama za vidole na gharama za kupambana na ugonjwa wa Covid-19 pamoja na kuendelea kupanua mtandao wa huduma.

Kwa siku zilizopita, Vodacom imekuwa na mwenendo mzuri wa ufanisi mwaka jana ilitoa jumla ya Sh54.5 bilioni kama gawio na Sh400 bilioni zilitolewa kama gawio maalumu ambalo ni sawa na Sh178.57 kwa hisa moja.

Kwa mujibu wa taarifa za fedha za kampuni hiyo za hivi karibuni, mapato na faida yake vitaendelea kuzorota endapo hawatamaliza mizozo ya kikodi baina yao na TRA au Mahakama ya kodi.

Chanzo: Mwananchi

  • Share:
author avatar
Admin

Previous post

No more worries as TRA assures Arusha taxpayers
July 20, 2021

Next post

Vikwazo vinavyokwamisha watu kuanzisha biashara vyatajwa
July 20, 2021

You may also like

OTMI8038
PUNGUZO LA RIBA MIKOPO KWENYE KILIMO IWE NJIA ISIYOISHIA NJIANI
2 February, 2022
Yellow and Black Quotes Facebook Post (1)
Lifted ban on pregnant girls in Tanzania.
26 November, 2021
Yellow and Black Quotes Facebook Post
The sooner African people can realize that economic emancipation has come through AfCFTA, the better.
23 November, 2021

Leave A Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MOST POPULAR

depositphotos_41972755-stock-photo-capitalism-3d-sphere-word-cloud-1024×675
April 3, 2019
Freedom & Prosperity: The two cornerstones which keeps capitalism essential even today
Read More

RESEARCH & REPORT

Starting Busines Report in Tanzania 2021-2022

Starting Busines Report in Tanzania 2021-2022

Doing Business measures aspects of business regulation affecting small...

FEATURED ANALYSIS

PUNGUZO LA RIBA MIKOPO KWENYE KILIMO IWE NJIA ISIYOISHIA NJIANI

PUNGUZO LA RIBA MIKOPO KWENYE KILIMO IWE NJIA ISIYOISHIA NJIANI

 Na Amani Mjege Mnamo tarehe 24 january 2022 Benki...

Lifted ban on pregnant girls in Tanzania.

Lifted ban on pregnant girls in Tanzania.

It has never been more evident than it is...

The sooner African people can realize that economic emancipation has come through AfCFTA, the better.

The sooner African people can realize that economic emancipation has come through AfCFTA, the better.

Kenya and Tanzania are restoring the once-decayed faith in...

CHUNGU TAMU: BILIONI 100 ZILIZOTENGWA NA NMB KUWAKOPESHA WAKULIMA, WAVUVI NA WAFUGAJI

CHUNGU TAMU: BILIONI 100 ZILIZOTENGWA NA NMB KUWAKOPESHA WAKULIMA, WAVUVI NA WAFUGAJI

Oktoba 7 mwaka 2021 jijini Dar es saalam, Bank...

People should be educated not to fear competition.

People should be educated not to fear competition.

4th discussion; IDEAS CLUB, Last Saturday, with great enthusiasm,...

VIKWAZO VYA KIBIASHARA KUONDOLEWA: WADAU SEKTA YA UCHUMI KENYA NA TANZANIA WATUMIE VYEMA  FURSA HII

VIKWAZO VYA KIBIASHARA KUONDOLEWA: WADAU SEKTA YA UCHUMI KENYA NA TANZANIA WATUMIE VYEMA FURSA HII

Tanzania na Kenya zimefanikiwa kuondoa  vikwazo 12 vya biashara...

Kuelekea Uchumi wa Buluu: SHERIA NA KANUNI ZA UVUVI LAZIMA ZIANGALIWE UPYA

Kuelekea Uchumi wa Buluu: SHERIA NA KANUNI ZA UVUVI LAZIMA ZIANGALIWE UPYA

Uchumi wa Buluu unajumuisha shughuli zote za uendelezaji na...

Recognizing the contribution of entrepreneurship to the economy.

Recognizing the contribution of entrepreneurship to the economy.

3rd Meeting Our IDEA club had a great weekend...

JOIN OUR NEWSLETTER

Stay connected with what our team is accomplishing; subscribe today and get the full report and updates, straight to your inbox, every month.
You may also receive information and direct marketing from us, but you may update your preferences at any time.

Liberty Sparks

  • Sinza Kijiweni
  • Dar es Salaam, Tanzania
  • T +255763855554
Facebook Twitter Youtube Instagram Linkedin Google-plus-g

A Freer, Flourishing Society

About

  • Our Story
  • People
  • What we do
  • Jobs & Internships
  • Annual Reports & Financials
  • FAQs
  • Contact
Menu
  • Our Story
  • People
  • What we do
  • Jobs & Internships
  • Annual Reports & Financials
  • FAQs
  • Contact

Grants+Awards

  • Grants
  • Awards
  • FAQs
Menu
  • Grants
  • Awards
  • FAQs

Events

Training

  • Overview
  • Certifications
  • Upcoming Courses
  • Think Tank Shark Tank
  • FAQs
Menu
  • Overview
  • Certifications
  • Upcoming Courses
  • Think Tank Shark Tank
  • FAQs

COPYRIGHT © 2021 LIBERTY SPARKS

Login with your site account

Lost your password?

Not a member yet? Register now

Register a new account

Are you a member? Login now

[ Placeholder content for popup link ] WordPress Download Manager - Best Download Management Plugin